Trump kuufunga mtandao wa TikTok inchini Marekani

Rais wa Marekani Donald Trump amesema jumamosi hii ataufunga rasmi mtandao wa TikTok (Mtandao wa Kijamii ambao unamilikiwa na Wachina) na kamwe hautotumika nchini Marekani.

“Nitaipiga marufuku TikTok kutumika hapa Marekani na Mamlaka hayo ninayo na sitaki Kampuni za Marekani zinunue mtandao huo (baada ya Microsoft kuonesha nia ya kuinunua TikTok)” -TRUMP

TikTok inatajwa kuwa tishio kwa usalama na Wamarekani kwa kile kinachodaiwa kuwa Serikali ya China inautumia mtandao huo kudukua na kufuatilia mawasiliano ya Raia wa Marekani na maeneo mengine wanaotumia mtandao huo na kusema huenda ukatumika kuingilia uchaguzi.