Tumieni petroli kusafishia barakoa- Rais wa Ufilipino

Rais wa Ufilipino Rodrigo Duterte leo amewaambia raia wake watumie petroli kusafisha barakoa(mask) huku akiwasisitizia kwamba ushauri wake huo sio mzaha.

Duterte amesema dawa za kuua vijidudu zikikosekana, petroli inaweza kutumika kama mbadala.

Wataalamu wa afya hata hivyo wamesema ushauri huo wa kusafisha barakoa haufai, agizo la kuvaa barakoa lilitolewa mnamo mwezi Machi nchini Ufilipino, Taifa ambalo tayari limethibitisha maambukizi yapatayo 90,000 ya viruisi vya corona na zaidi ya vifo 2,000.