Bilionea wa Nigeria awazawadia watoto wake magari ya Ferrari Portofino


Hatua ya bilionea Femi Otedola kuwanunulia mabinti zake watau magari ya kifahari imezua gumzo katika mitandao ya kijamii nchini Nigeria.

Femi Otedola, ambaye ni tajiri mkuwa katika sekta ya mafuta, aliwazawadia mabinti zake magari aina ya Ferrari Portofino.

Florence Ifeoluwa Otedola anayefahamika kwa jina maarufu kama DJ Cuppy aliweka mtandaoni picha ya magari waliyonunuliwa na baba yao siku ya Jumatano.

Aliandika baba yao amenunua magari matatu kwa watoto wake watatu- Tolani, Temi na Ifeoluwa Otedola.

Data kutoka kwa Wikipedia inaonesha Femi Otedola ana mali ya zaidi ya dola bilioni 1.85 za Kimarekani.

"Baba yetu alitupeleka dukani na kutununulia kila mtu gari lake!", kwa mujibu wa ujumbe uliowekwa kwenye Twitter na Temi Otedola.



Post a Comment

0 Comments