Lowassa amuambia Rais Magufuli “inatisha lakini usitishike, umma na dunia inajua”

 

“Sina mashaka juu ya Rais Magufuli kushinda, mashaka yangu ni atashinda kwa kura ngapi?, huko wameanza kujipambanua sana, maneno mengi, fujo zile wanaonekana kwenye Mitaa, ma-TV pengine ina tishatisha lakini tumemuambia Rais wetu usitishike hata kidogo, umma wa Watanzania upo nyuma yako na dunia inajua” Waziri Mkuu Mstaafu Lowassa

“Nasema hivyo sababu kama umesikiliza TV leo, Australia Rais anajiuzulu, Bolvia Rais anajiuzulu kote sababu ya Corona, si mchezo, nyinyi mtu wenu tena mtu mweusi hana nguvu za Mitume anawaambia Taifa lake jamani tumuende MUNGU tumuombe tuepukane na hili janga, watu wa ajabu wakasema anababaisha, tumepita wiki mbili wiki tatu hamna Corona” Waziri Mkuu mstaafu Edward Lowasaa

Post a Comment

0 Comments