Moto usio kuwa na chanzo wamuunguza mwanafunzi wakati akielekea shuleni

Na Amiri Kilgalila,Njombe
Katika hali isiyo ya kawaida mwanafunzi wa shule ya sekondari Madilu iliyopo wilayani ludewa mkoani Njombe wa kidato cha kwanza Roida Mwabena,a mejikuta katika wakati mgumu mara baada ya sare ya shule aliyovaa kuanza kuungua moto wakati akiwa njiani kuelekea shuleni ,huku chanzo cha moto huo kikiwa hakijulikani.

Roida Mwabena mtoto aliyekumbwa na kadhia hiyo anasema alishangaa ghafla kuona moto mkubwa unawake kwenye mavazi yake na kuamua kuamu kukimbia akirudi kwa baba yake mkubwa.

“Mimi niliona moto unawake nikarudi nakimbia kwa baba mkubwa akanitoa sketi akauzima ule moto”alisema moto Roida Mwabena

Mwalimu mkuu wa shule hiyo Bw.Michael Mwalongo amesema tukio hilo limemkuta mwanafunzi majira ya saa kumi na mbili asubuhi kwani mtoto huyo amekuwa akitokea nyumbani kulingana na hali yake ya afya huku baadhi ya wanafunzi wengine wakiishi hosteli.

“Mtoto akiwa njiani ndio tukio hilo limemkuta,hivyo ameungua sketi ya shule na sweta moto ule wasamalia wema walijaribu kuuzima na baadaye wakamleta shule,kumchunguza akawa ameungua na mkono baada ya hapo mzazi akaja kumchukua na piki piki na kumpeleka kituo cha afya”alisema Michael Mwalongo

Kwa upande wake mganga mkuu wa kituo cha afya  madilu,Salmini magunja amekiri kumpokea mwanafunzi huyo ambaye alifikishwa zahanati kwa ajili ya matibabu huku nguo zake zikiwa zimeungu pamoja na mwanafunzi kuwa na majeraha ya moto.

“Tulimpokea na kweli na yunifomu zilikuwa zimeungua moto na yeye kuna baadhi ya maeneo ya mwili kidogo ulishika moto,tulimuuliza labda ulitembea na kiberiti alisema hapana,na hapa tumempa matibabu ya kawaida kama mtu aliyeungua moto japo hili ni jambo la ajabu mpaka ndugu zake wameshangaa,lakini kwasababu hali yake ni nzuri tumemruhusu aende nyumbani”alisema Salmini Magunja

Kutokana na hali kituo hiki kimemtafuta baba mzazi wa mtoto huyo Andrea Mwabena ambaye amekiri mtoto wake kukumbwa na tatizo hilo la kustaajabisha.

“Tukio limemkuta mtoto asubuhi,na sisi tunashangaa kwa kweli ndio maana tumekaa tuangalie nini chanzo cha huu moto,kwasababu moto ukianza kuwaka bila chanzo ni tatizo na ukiangali hili tukio la moto ni la kwanza hatujawahi kuona”alisema Andrea Mwabena baba wa mtoto huyo

“Yaani na mimi silielewi hili tatizo mpaka saizi kwa motto aliaga vizuri asubuhi akaondoka lakini nikaona baba ake ananipigia simu anasema mama njoo huku moto anawaka moto”alisema Regina Mnyanga mama wa mtoto

Vile vile mwalimu mkuu wa shule ya sekondari Madilu amesema tukio la aina hiyo limekuwa la kwanza kutokea katika shle hiyo licha ya kuwepo kwa matukio mengine ya ajabu kama watoto kuzimia.

“Hili ni tukio limetushangaza lakini alikuwa akizimia mara kwa mara,na hili la kupoteza fahamu siku mbili mpaka tatu ni kawaida lakini hili la moto tumeshangaa”alisema mwalimu  Michael Mwalongo