RC Mtwara ahahidi kuwpa ofisi Boda boda


Na Faruku Ngonyani, Mtwara.

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Gelasius Byakanwa amehaidi kuwapa ofisi madereva Bodaboda ili wapate sehemu ya kukutana na kujadili masuala yao.

Ameyazungumza hayo wakati wa uzinduzi wa mashindano ya Mpira wa Miguu kwa madereva hao pikiki Mkaoni hapo aliyoyazindua uwaanja wa Nangwanda Sijaona uliopo Manispaa Mtwara Mikindani.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema kuwa Mashindano hayo yameanzishwa kwa lengo la kuwakutanisha Madereva Pikipiki (BODABODA) na kuzifahamu changamoto wanazokumbanananzo wawapo Barabarani.

‘kuna vipaji vingi tunavipoteza na tunavipoteza kwa sababu hatuna timu ambayo inatuonyesha hivyo vipaji,sasa kupitia michezo hii tunaona vipaji vilivyojificha kutoka kwa hawa bodaboda’

Kwa upande wa Mwenyekiti wa Bodaboda Mkoa wa Mtwara Ndg Omari Nassoro Mbonde amesema kuwa mashindano hayo yamekuja muda muafaka kwani kupitia michezo hiyo watapata fursa ya kujenga uhusiano wao lakini pia itakuwa sehemu ya kujua changamoto wanazo kumbananzo.

Mashindano hayo kwa waendesha pikipik (BODABODA) imezindiliwa hii leo Tarehe 15 Sepemba 2020 na inatarajia kukamilika Noemba 04 mwaka huu 2020.

Katika mashindano hayo zawadi kwa mshindi wa kwanza itakuwa milioni mbili na laki tano(2,500,000) atakaeshika nfasi ya pili atajipatia fedha shilingi milioni moja na laki tano (1,500,000 ) na kwa atayeshika nafasi ya tatu atapata shilingi Milioni moja (1,000,000)

Mashindano hayo ya Madereva pikipik maaruku kama Bodaboda yamehusisha Timu kumi na nane (18) kuotoka Wilaya zote zilizopo Mkoani Mtwara.

Post a Comment

0 Comments