TCRA imekifungia Wasafi FM kwa muda wa siku saba

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imekifungia kituo cha utangazaji cha Wasafi FM kwa muda wa siku saba kuanzia Septemba 12 hadi Septemba 18 mwaka huu.

Hatua hiyo imefikiwa baada ya kituo hicho kukiuka kanuni za Mawasiliano ya kielektroniki na posta katika utangazaji wa radio na televisheni za mwaka 2018 ambazo zinamtaka mtangazaji kutangaza maudhui ya staha.

Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Mhandisi James Kilaba amesema kuwa ukiukwaji huo wa kanuni uliofanyika katika vipindi vya The Switch na Mashamsham, utasababisha kituo hicho kusitisha huduma za utangazaji kwa muda wa siku saba na kuomba msamaha kwa siku ya leo.

Aidha adhabu hiyo si kwamba itakuwa aina hiyo kwa wote, bali inaweza kubadilika.

Mwanzoni mwa mwezi huu, chombo kingine cha habari Clouds media kilifungiwa kwa kukiuka kanuni ndogo za uchaguzi.