Tetesi za soka kimataifa


 Manchester United itapaswa kulipa kiasi cha pauni milioni 18.5 pekee ikiwa wanataka kumsajili winga wa Real Madrid na Wales Gareth Bale, 31.(Mundo Deportivo - in Spanish)

Tottenham inapenda kumpata mshambuliaji wa Southampton, Muingereza Danny Ings, 28. (Football.London)

Douglas Costa amewekwa tayari kuuzwa na Juventus. Manchester United awali walikuwa wakihusishwa na taarifa za kumtaka winga huyo wa Brazil, 29. (Goal)

Kiungo wa kati wa Denmark Christian Eriksen, 28, anaweza kuruhusiwa kuondoka Inter Milan ikiwa ni miezi kadhaa tu tangu kujiunga akitokea Tottenham. (Calciomercato - in Italian)

Arsenal inataka kumsajili mlinda mlango wa Iceland Rinar Runarsson, 25, na imeanza mazungumzo na Dijon kuhusu mpango huo. (Telegraph)

Porto imepunguza gharama ya kumnasa beki wa kushoto Mbrazili Alex Telles mpaka pauni milioni 18.5, huku Manchester United ikimtaka mchezaji huyo, 27. (A Bola - in Portuguese)

Tottenham inaweza kuchuana na Manchester United kupata saini ya Beki wa kushoto wa Real Madrid, Mhispania Sergio Reguilon,23. (Mail)

Spurs wako kwenye mazungumzo na Trabzonspor kwa ajili ya mpango wa kumpata mshambuliaji Alexander Sorloth. Mchezaji huyo, 24 anacheza kwa mkopo wa miaka miwili akitoka Crystal Palace. (Express)

Tottenham imeingia kwenye kinyang'anyiro cha kumsajili Hellas Verona na beki wa kati Marash Kumbulla. Chelsea na Manchester United wamehusishwa na taarifa za kutaka kumnasa mchezaji huyo, 20. (L'Arena, via Sun)

Spurs wako kwenye mazungumzo na Trabzonspor kwa ajili ya mpango wa kumpata mshambuliaji Alexander Sorloth

Newcastle inataka kumchukua winga wa Roma na Uturuki Cengiz Under kwa mkopo. Leicester pia inavutiwa na mchezaji huyo wa miaka 23. (Inside Futbol)

Bournemouth imeiambia Leicester kuwa watapaswa kulipa pauni milioni 50 kumpata kiungo wa kati David

Post a Comment

0 Comments