Watu 77 wamefariki katika mafuriko nchini Nigeria

 


Mafuriko yaliotokea nchini Nigeria yamepelekea vifo vya watu  77.

Mvua kali zilizonyesha nchini humo zimepelekea mafuriko   yaliosababisha uharibifu.

Idadi ya vifo kutokana na   mvua hizo zilizopelekea mafuriko  imeripotiwa kuongezeka na kufikia watu  77.

Msemaji  wa kitengo kinachohusikana na kutoa huduma ya kwanza katika eneo hilo SEMA,  Umar Muhammed ametangaza vifo vya watu  wanane  na wengine 17 kujeruhiwa  kutokana na uharibifu uliopelekea mafuriko hayo.

Idadi ya vifo kutokana  na mafuriko  hayo inazidi kuongezeka.

Majumba zaidi ya 25 961 yameporomoka na maji ya mafuriko huku ikiripotiwa kuwa  mashamba na mazao pia  vimeharibiwa na maji katika eneo la hekari zaidi ya 7019.

Msemaji  huyo  ameendelea kuwa ametolea wito serikali kuomba msaada kwa ajili ya waathirika wa mamfuriko hayo yaliotokea nchini Nigeria kutokana na mvua kali.

Post a Comment

0 Comments