Waziri wa Ulinzi wa Kitaifa Hulusi Akar alikutana na Waziri wa Ulinzi wa Indonesia Prabowo Subianto.
Kulingana na taarifa kutoka kwa Wizara ya Ulinzi, iliarifiwa kuwa Subianto alikuwa amekuja Uturuki kufuatia mwaliko rasmi, na kupokewa kwa gwaride la heshima lililoandaliwa na jeshi.
Baada ya kumaliza mazungumzo ya ana kwa ana, Akar na Subianto waliongoza mkutano baina ya wajumbe kutoka pande zote.
Kwenye mikutano hiyo ya mazungumzo, viongozi walitoa maoni na kubadilishana mawazo juu ya maswala ya ulinzi na usalama wa pande mbili na wa kikanda, na kuweka ushirikiano katika sekta ya ulinzi.
0 Comments