Rais mteule wa Marekani Joe Biden aibuka na ushindi Georgia baada ya kura kuhesabiwa tena huku juhudi za kuchukua mkondo wa kisheria za Donald Trump zikiendelea katika majimbo matatu zikiendela.
Chama cha Democratic kimeshinda chama pinzani cha Republican huko Georgia kwa kura 12,284 kama inavyohitajika katika sheria ya kuhesabu kura tena.
Bwana Biden amesema Bwana Trump alijua kuwa hatashinda na alionesha "kutowajibika kwa kiwango cha juu" kutokiri kuwa ameshindwa.
Rais wa chama cha Democratic amejipanga kuchukua nafasi Januari kama rais wa 46 wa Marekani.
Ushindi wa Bwana Biden katika wingi wa kura hadi kufikia sasa ni milioni 5.9.
Katika kura za majimbo ambazo ni lazima kushinda ili kuwa rais wa Marekani, Biden alipata kura 306 dhidi ya Trump aliyepata kura 232 akiwa amepita zile zinazohitajika.
