China: Marufuku kutembea na mbwa hadharani

Kaunti moja nchini China huko Yunnan imelazimika kufikiria tena sera ya kupiga marufuku wakazi wa eneo hilo kutembea na mbwa katika maeneo ya umma kuanzia Novemba 20.

Taarifa hiyo imesema, yeyote atakayekutwa anatembea na mbwa hadharani mara tatu, mbwa wake atachukuliwa na mamlaka na kuuawa.

Maafisa wamesema hiyo ni hatua ya kulinda wakazi kwasababu kumekuwa na matukio ya mara kwa mara ya mbwa kuuma watu.

Hata hivyo, sera hiyo imekasirisha watu katika mitandao ya kijamii huku maafisa wakisema huenda "wakafikiria tena" hatua hiyo.

Taarifa hiyo inasema kuanzia Novemba 13, itakuwa ni lazima kwa wamiliki wote kusalia na mbwa wao nyumbani muda wote.

Pia imeongeza kwamba sera hiyo inatoa muongozo mzuri wa kuishi na mbwa.

 

Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items