Jifunze namna ya kutenda wema kwa wengine

 


Kisa cha baba ambae alikuwa akitembelea mashambani na mwanawe. Katika kutembea kwao wakakuta kiatu kimoja chakavu ambacho anaonekana mwenyewe ni masikini sana.

Mwana  akamwambia Baba yake, unaonaje kama tutamfanyia mzaha huyu mwenye kiatu, tukifiche hiki kiatu kisha sisi wenyewe tujifiche halafu tuangalie mwenyewe akirudi atafanyaje ili tumcheke?

Yule  Baba akamjibu "Hatutakiwi kujifurahisha kwa kuwaudhi wengine" lakini wewe kijana wangu ni tajiri unaweza kufanya kitu kikakufurahisha wewe mwenyewe na kikamfurahisha huyu bwana mwenye kiatu pia."

Kijana akamuuliza baba yake kivipi!?
Baba akamwambia;Badala ya kukificha kile kiatu, unaweza kukiacha palepale na ukaingiza pesa ndani yake.Kisha tujifiche ili uone athari yake.

Mwana  akafurahishwa na rai ya  Baba yake na akafanya kama alivyoelekezwa, kisha  wakajificha nyuma ya miti.

Sio muda mrefu akarudi yule masikini ili achukue kiatu chake. Tahamaki anakuta pesa ndani ya kiatu kile na pesa kama ile katika kiatu kingine.

Akaziingiza pesa mfukoni na akapiga magoti kusujudu hali yakuwa ni mwenye kulia, kisha akamwambia Mungu kwa sauti ya juu : "Ninakushukuru Ewe Mungu wangu, Ewe ambae umejua kwamba mke wangu ni mgonjwa na wanangu wana njaa hawana mkate, ukaniokoa mimi na watoto wangu."

Kijana wa tajiri aliathirika sana kwa kuona huruma zaidi na macho yake nayo yakajaa machozi ya furaha kuona amemsaidia mtu mwenye uhitaji.

Hapo ndipo yule  Baba akamwambia nwanawe  "huoni kwamba sasa una furaha zaidi kuliko vile ulivyotaka kufanya mwanzo"?
Mwana  akajibu nimejifunza  Na  sitoisahau muda nitakao kuwa hai.

Hivi sasa nimejifunza kitu kwamba ukitoa utakuwa na furaha zaidi kuliko ukizuia au ukichukua.
Baba akasema kama hivyo ndivyo basi unatakiwa ujue kwamba,  kutoa ni SADAKA na kuna namna nyingi.

Kumsamehe mtu pamoja na uwezo wa kumuadhibu unao ni  SADAKA .
Kumuombea dua ndugu yako bila yeye mwenyewe kujua ni  SADAKA.
Kumpa ndugu yako udhuru na ukamuondolea dhana mbaya ni  SADAKA .
Kumchungia heshima ndugu yako  wakati hayupo ni  SADAKA .
kushare ujumbe huu na ndugu zako pia ni  SADAKA .

Post a Comment

0 Comments