Mabingwa watetezi wa michuano hiyo klabu ya Bayern Munich, imepangwa kuanza kucheza ugenini dhidi ya Lazio ya Italia Ilihali miamba ya soka ya Uhispania klabu ya Barcelona, uso kwa uso na PSG, miamba ya soka kutoka nchini Ufaransa ikiwa ni vita ya Messi dhidi ya Neymar Junior.
Borussia Monchengladbach ya Ujerumani kuvaana na Manchester City ya Uingereza, vijana watukutu wa Diego Simeone Atletico Madrid ya Uhispania watavaana na Chelsea ya Uingereza chini ya Kocha Frank Lampard.
Dortmund ya Ujerumani watasafiri hadi nchini Uhispania kuwafuata klabu ya Sevilla, wakati RB Leipzig ya Ujerumani wataumana na Liverpool ya Uingereza, FC Porto ya Ureno dhidi ya Juventus ya Italia ya CR7.
Michezo ya hatu ya 16 bora inatazamiwa kuanza kuchezwa tarehe 15 na 16 hadi tarehe 23 na 24 mwezi Februari, kwa michezo ya mzunguko wa kwanza na michezo ya marudiano kuchezwa tarehe 9 na 10 hadi tarehe 16 na 17 mwezi machi mwaka 2021.
Monchengladbachi v Manchester City.
Lazio v Bayern
Atletico v Chelsea
Leipzing v Liverpool
Porto v Juventus
Barcelona v PSG
Sevilla v Dortmund
Atlanta v Real Madrid
0 Comments