Iran yaunga mkono uamuzi wa Marekani dhidi ya Saudia

 


Msemaji wa Wizara ya Mambo ya nje ya Iran Said Hatibzade amesema uamuzi wa Marekani kukata msaada wake wa kijeshi kwa Saudi Arabia katika vita huko Yemen "inaweza kuwa hatua ya kurekebisha makosa ya zamani".


Katika taarifa iliyotolewa na Wizara ya Mambo ya nje, Hatibzade alisema kwamba wanaunga mkono uamuzi wa utawala wa Marekani nchini Yemen.


Hatibzade, aliongeza kwa kusema,


"Ikiwa uamuzi wa kuacha kuiunga mkono Saudi Arabia na kutowauzia silaha sio ujanja wa kisiasa, basi itakuwa hatua ya kurekebisha makosa ya zamani.".


Akisisitiza kwamba uamuzi pekee hautatosha kumaliza mzozo wa Yemen, Hatibzade alisema.


"Iran inakaribisha kila juhudi ya jamii ya kimataifa kuunga mkono Yemen na kupunguza msaada kwa wavamizi.".


Akitoa wito kwa nchi zingine ambazo zinaunga mkono Saudi Arabia kukata msaada wao, Hatibzade alibainisha kuwa nchi zinazoongozwa na Saudi Arabia zinapaswa kuacha mashambulizi.

Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items