Jamii ya Wayazid kutoka Kaskazini mwa Iraq wameileta miili ya watu wao 104 waliouliwa na kikundi cha Islac State wakati wa utawala wa kigaidi mwaka 2014.
Mabaki ya miili yao yametambuliwa na kufufuliwa kutoka kwenye makaburi ya pamoja na kuzikwa katika kijiji cha Kocho kilichopo karibu na Mlima Sinjar katika jimbo la Ninevah.
Maelfu ya wanaume waliuawa na wanawake na watoto kutumikishwa kama watumwa na kubakwa wakati IS walipochukua eneo la Wayazid.
Umoja wa Mataifa unasema kuwa IS walitekeleza mauaji ya kimbari dhidi ya jamii ya Yazid.
Wayazid ni wafuasi wa wa dini yenye mchanganyiko wa imani ya kale ya dini ya Wairan, dini ya Kibudha, Ukristo, na Uislamu.
Wanachukuliwa na IS- ambalo ni kundi la jihadi la Sunni kama wafuasi wa dini ya uzushi.
Iliaminiwa kuwa walikuwepo Wayazidi wapatao 550,000 waliokua wakiishi Iraq kabla ya kuvamiwa na IS tarehe 3 Agosti, 2014. Wayazidi wapatao360,000 Yazidis walitoroka na kupata hifadhi katika maeneo mengine.
