Mama alietelekezwa na watoto wawili wenye ulemavu apatiwa msaada wa Mabati

 


Na John Walter-Babati

Kituo cha Msaidie mlemavu awaze kujitegemea (MMA) kilichopo chini ya kanisa katoliki parokia ya Galapo wilayani Babati Mkoani Manyara kimetoa msaada wa mabati kumi kwa familia ya Bi. Anastazia Aribogasti  ambaye ametelekezewa watoto wawili ambao wana ulemavu wa viungo.


Hata hivyo tayari mama huyo ameshaanza kujenga msingi wa nyumba yake pamoja na kufyetua matofali.


Akizungumza wakati wanapotoa msaada huo katibu wa shirikisho la watu wenye ulemavu mkoa wa Manyara Peter Sanka amesema walimfuatilia baba huyo ambaye ameitelekeza famalia hiyo na kuondoka na watoto wengine ambao hawana ulemavu kwa ajili ya kuendelea kuitunza familia bila mafanikio.


Aidha Katibu huyo ameiomba jamii kushirikiana kwa pamoja katika kuiwezesha familia hiyo kwa kuwa  jamii ndiyo walezi pekee wa familia hiyo kwasasa.


Kwa upande wake padri wa Parokia ya Galapo George Kamula amewaomba watu kuwa na utamaduni wa  kuwasaidia watu ambao wanapitia kwenye mazingira  magumu kwani kwa kufanya hivyo ndiyo namna ya kuwapa faraja na kuwaonyesha upendo  kwa vitendo.


Naye mwenyekiti wa kijiji cha Hala Theofili John amewataka wananchi kushikamana na kwa pamoja ili kuweza kuwasaidia watu wenye uhitaji na kuachana na dhana ya kutegemea misaada kutoka nje pekee kwani kila mtu anaweza kufanya hivyo.


Bi.Anastazia Aribogasti mara baada ya kupatiwa msaada huo amewashukuru wishukuru serikali na wadau waliofanikisha kumsaidia kupata msaada huo wa mabati kumi.

Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi