UN yatuma timu Libya

 


Umoja wa Mataifa (UN) umepeleka timu ndogo kusaidia utaratibu wa ufuatiliaji wa mapigano nchini Libya.


Katika mkutano wa kila siku na waandishi wa habari, Msemaji Mkuu wa Katibu Mkuu wa UN Stephane Dujarric amesema timu hiyo iliwasili nchini humo jana usiku na itaunga mkono utaratibu wa ufuatiliaji wa mapigano unaoongozwa na Libya kwa kushauriana kwa karibu na tume ya jeshi ya 5 + 5.


Dujarric hakutoahabari kuhusu timu ngapi zilipelekwa Libya.


UN ilitangaza kuwa itapeleka waangalizi wa kimataifa nchini Libya kuhakikisha usitishaji wa mapigano wa kudumu na kudhibiti vita.


Kamati ya Pamoja ya Kijeshi ya 5 + 5 ilikuwa imeomba kupelekwa kwa waangalizi wa kimataifa wasio na silaha na sare nchini Libya chini ya usimamizi wa UN.

Post a Comment

0 Comments