Mourinho Kocha Mpya AS Roma


Baada ya kufukuzwa kazi mwezi uliopita akiwa Tottenham Hotspurs Jose Mourinho ametangazwa kuwa Kocha mpya wa AS Roma ya Italia na atarithi mikoba ya Paulo Fonseca anayeondoka mwisho wa msimu.

Hii ni mara ya pili kwa Kocha Jose Mourinho kufanya kazi Italia kama Kocha, baada ya kudumu kwa misimu miwili na Inter Milan na baadae 2010 akajiunga na Real Madrid ya Hispania.

Akiwa Inter Milan Jose Mourinho alifanikiwa kushinda taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya pamoja na Ligi Kuu Italia Serie A.

Post a Comment

0 Comments