Wanachama wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wamelaani tabia ya Korea Kaskazini, kufuatia majaribio ya karibuni ya makombora yaliofanywa na taifa hilo.
Wawakilishi wa Ufaransa, Ireland na Estonia
katika Umoja wa Mataifa, wamesema ufyatuaji wa makombora hayo ulikuwa
sehemu ya mfano wa uchokozi wa Korea Kaksazini.
Mabalozi hao wametoa
wito kwa taifa hilo kuheshimu vikwazo ilivyowekewa na Umoja wa Mataifa.
Marekani na Uingereza pia zilielezea hisia sawa. Baraza la usalama
lilikutana mjini New York kujadili hali hiyo katika kikao cha faragha,
lakini awali, hakukuwa na taarifa ya pamoja.
0 Comments