China yapinga kampuni zake kuwekewa vikwazo na Marekani


China kupitia msemaji wa wizara ya uchumi Shu Jueting, imepinga vikali vikwazo dhidi ya kampuni za China ikisema vikwazo hivyo havina maana. 


Amesema China itawasilisha mapingamizi yake kwa Marekani juu ya suala hili na itafanya kila iwezalo kutetea kampuni zake dhidi ya kuwekewa vikwazo.


Serikali ya Marekani hapo jana Jumatano iliziweka kampuni za China katika orodha ya marufuku ya biashara kufuatia wasiwasi wa usalama wa taifa na sera za kigeni.

Post a Comment

0 Comments