https://monetag.com/?ref_id=TTIb Takriban watu 22 wauawa katika shambulizi katika kambi ya DR Congo | Muungwana BLOG

Takriban watu 22 wauawa katika shambulizi katika kambi ya DR Congo

 


Takriban watu 22 wameuawa katika shambulizi kwenye kambi ya watu waliokimbia makazi yao katika jimbo la Ituri mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.


Shambulio hilo limelaumiwa kwa kundi la Cooperative for the Development of the Congo (Codeco) ambalo linasemekana kufyatua risasi kwenye kambi hiyo.


Watu 20 walizikwa mara moja katika makaburi mawili ya kawaida, huku wengine wawili wakizikwa baadaye, shirika la habari la AFP lilimnukuu afisa wa Msalaba Mwekundu akisema.


Shambulio kwenye kambi hiyo hiyo wiki iliyopita liliua watu 29.


Ituri na jimbo jirani la Kivu Kaskazini ziliwekwa chini ya hali ya kuzingirwa tarehe 7 Mei - kwa mamlaka kukabiliana na ukosefu wa usalama katika eneo lililosababishwa na makundi yenye silaha ikiwa ni pamoja na Codeco na Allied Democratic Forces (ADF).


Kama sehemu ya kuzingirwa, maafisa wa kijeshi walichukua nafasi za maafisa wa kiraia waliokuwa wakisimamia utawala wa eneo hilo.


Post a Comment

0 Comments