Rwanda yathibitisha kuwa na visa sita vya aina mpya ya corona- Omicron

 




Serikali ya Rwanda imethibitisha kuwa visa sita vya aina mpya ya virusi vya corona aina ya Omicron.


Imesema visa hivyo viligundulika katika sampuli zilizokusanywa kutika kwa wasafiri pamoja na watu wengine waliokutana na wasafiri hao, kulingana na taarifa ya wizara ya afya.


Imesisitiza haja ya watu wote wenye umri wa miaka 12 na zaidi kupata chanjo kamili na wale wenye umri wa miaka 18 na zaidi kuangalia uwezekano wa kupata chanjo ya kuboresha chanjo za awali.


Rwanda imekwishawachanga asilimia 40 ya watu wake na hivi karibuni ilianza kutoa chanjo ya kuimarisha kinga ya chanjo za awali.




Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi