Vital Kamerhe aachiwa kwa dhamana DR Congo

 


Aliyekuwa wakati mmoja mkuu wa wafanyakazi wa umma nchini DR Congo Vital Kamerhe ameachiliwa huru kufuatia agizo la mahakama.


Kiongozi huyo ameachiwa huru Jumatatu usiku baada ya kukata rufaa dhidi ya kifungo alichokuwa akihudumia.


Vital Kamerhe hatahivyo alilazimika kulipa $500,000 kama dhamana.


Hadi kufikia sasa alikuwa amehudumu kifungo cha mwaka mmoja na miezi saba jela kati ya kipindi cha miaka 13 aliohukumiwa .


Awali Kamerhe ambaye aliamua kufanya kazi na rais Felix Tshisekedi alihukumiwa kifungo cha miaka 20 jela kwa wizi wa $ 48.831m fedha za uma .


Hatahivyo kifungo hicho kilipunguzwa na kufikia miaka 13 jela baada ya kukata rufaa.


Akiwa mkaazi wa mji wa Bukavu mashariki mwa DRC , Kamerhe alikuwa mwandani mkuu wa rais Feliz Tshisekedikatika uchaguzi wa urais wa Disemba 2018.


Akiwa mgombea , wa urais katika uchaguzi huo , alijiondoa na kuamua kumuunga mkono rais Felix Tshisekedi .


Wawili hao waliafikiana kwamba Kamerhe angeungwa mkono na Felix Tshisekedi katika uchaguzi ujao wa 2023.


Na punde baada ya kuachiwa kwake wafuasi wake walisheherekea

Post a Comment

0 Comments