Marekani yatoa taarifa kuhusu operesheni ya kijeshi ya China nchini Taiwan

 


Serikali ya Marekani imezungumza kuhusu mazoezi ya kijeshi ya China kwa siku ya pili karibu na kisiwa cha Taiwan.


‘’Hatua ya kijeshi ya China ni kubwa, ina athari, na bila uhalali wowote inasababisha mgogoro,’’ Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken alisema.


‘’Hakuna uhalali kwa matendo yao’’, aliendelea Blinken, akizungumza katika mkutano wa Asia.


China ilijibu ziara ya hivi majuzi nchini Taiwan na Spika wa Baraza la Wawakilishi la Marekani, Nancy Pelosi.


Ziara hiyo ambayo serikali ya Beijing ilikuwa imeonya kwa muda, na kufuatiwa na operesheni za kijeshi ambazo zimetatiza pakubwa Taiwan.


Marekani ilichukua hatua gani dhidi ya China?


Balozi wa China nchini Marekani, Qin Gang, aliitwa Ikulu ya Marekani jana kuhusu suala la nchi hiyo, kwa mujibu wa gazeti la Washington Post.


‘’Kufuatia hatua za Uchina, tumemwita Balozi Qin Gang kwenye Ikulu ya White House kuelezea vitendo vya uchochezi vya PRC [Jamhuri ya Watu wa Uchina],’’ msemaji wa Ikulu ya Marekani John Kirby aliambia gazeti hilo.


Hatua hiyo, inachukuliwa kuwa maandamano ya kidiplomasia.


Kirby aliongeza kuwa utawala wa Biden umekosoa hatua za kijeshi za China, ‘’ambazo ni kutowajibika dhidi ya lengo letu la muda mrefu la kudumisha amani na utulivu katika Mlango-Bahari wa Taiwan’’.

Post a Comment

0 Comments