China inalegeza vikwazo vya Covid baada ya maandamano


China inasema watu walio na dalili ya Corona isiyo kali sasa wataweza kutengwa nyumbani badala ya katika vituo vya serikali katika hatua ya kurahisisha sera yake ya Zero-Covid.


Watu hao sasa wataweza kujitenga nyumbani na kutuma ripoti ya matokeo ya vipimo.


Nchi pia imefuta mahitaji ya watu kufanyiwa vipimo vya PCR katika maeneo mengi ya umma isipokuwa hospitalini na shuleni.


Hatua hiyo inajiri wiki moja baada ya maandamano ya raia dhidi ya udhibiti wa janga la corona kuzuka kote nchini.


Masharti ya kuwaweka walio na virusi katika karantini za serikali ulikosolewa vikali sehemu kubwa ya watu wakilalamikia jinsi familia zilivyotenganishwa na wapendwa wao.


Baadhi ya watu waliokaidi amri hiyo walipelekwa karantini kwa lazima.


Video za mwaka mzima zimeonyesha walinzi wakiwatoa watu nje ya nyumba zao, ikiwa ni pamoja na picha za video kutoka Hangzhou wiki iliyopita ambazo zilionyesha mtu akipigana na maafisa.


Mabadiliko hayo ni ishara wazi kwamba China inaelekea kuachana na sera yake ya Zero Covid.


Nchi hiyo inakabiliwa na wimbi kubwa la maambukizi ya coro - zaidi ya 30,000 kila siku.

Post a Comment

0 Comments