DRC: Papa Francis awasihi waliodhulumiwa kusamehe, awataka wamuige Yesu

 


Papa Francis Jumatano aliwasihi watu wa Kongo kuwasamehe wale walio wadhuru, alisema hayo alipokuwa  akiongoza misa iliyohudhuriwa  na watu takriban milioni moja...


Papa Francis Jumatano aliwasihi watu wa Kongo kuwasamehe wale walio wadhuru, alisema hayo alipokuwa akiongoza misa iliyohudhuriwa na watu takriban milioni moja waliofurika kuhudhuria tukio kubwa la kwanza la papa Francis barani Afrika lenye lengo la kuleta amani na maridhiano kwa nchi iliyoathiriwa na miongo kadhaa ya ghasia.


Waumini wengi wa Kongo walikesha wakisubiri misa kwenye viwanja vikubwa kwenye uwanja wa ndege wa Ndolo walisubiri kuwasili kwa papa Francis, wakiimba , kucheza na wakiwa wamejawa na msisimko juu ya ujio wa kwanza wa papa tangu Mtakatifu John Paul wa Pili alipofanya ziara yake ya mwisho mwaka 1985.


Walishangilia wakati Francis alipoanza kuzunguka taratibu kwenye viwanja vya wazi akiwa katika gari lake la kipapa. Baadhi yao wakikimbia kando yake au kupeperusha bendera. Wanawake wengi walikuwa wamevalia magauni na sketi zilizoshonwa kwa vitenge vya waksi vyenye picha ya papa Francis au alama nyingine za kidini.


"Leo ninaelewa shauku ya bibi yangu wakati Papa John Paul II alipokuja," alisema Julie Mbuyi, mama wa watoto wawili mwenye umri wa miaka 45, ambaye alikuwa amevalia mavazi yaliyokuwa na ujumbe wa Francis. "Alifurahi sana kumuona na usiku ule kabla ya kuwasili kwa papa hakuweza kulala!"

Post a Comment

0 Comments