Msafara wa vikosi vya Umoja wa mataifa washambuliwa tena na umati wa watu DRC watatu wafariki

 



Watu watatu wamefariki dunia, na malori manne yaliteketezwa kwa moto katika shambulio lililofanywa na umati wa watu dhidi ya msafara wa vikosi vya Umoja wa Mataifa Jumanne jioni huko Minigi takriban kilomita 7 kaskazini mwa Goma, mashariki mwa DR Congo.


Vikosi vya Umoja wa Mataifa nchini DRC, Monusco, vimesema msafara huo ulikuwa unaelekea Goma wakati "watu waliokuwa wakiandamana" walifunga barabara "kwa mawe makubwa" kabla ya kuanza "kushambulia".


"Kwa bahati mbaya, watu watatu (raia) walikufa katika mzozo huo" wakati vikosi "vilikuwa vikijaribu kulinda msafara", taarifa ya kikosi hicho ilisema.


Maandamano mapya yametikisa Goma tangu Jumatatu, huku waasi wa M23 wakiukaribia mji huo kutoka magharibi.


Waandamanaji wanatoa wito kwa Vikosi vya Kanda ya Afrika Mashariki, na vikosi vya Umoja wa Mataifa kupambana na waasi.


Waasi wa M23 wamemshutumu Rais Felix Tshisekedi kwa "kuchochea machafuko" kwa kuunga mkono maandamano "badala ya kuhimiza amani" kwa njia ya mazungumzo.


Mamlaka ya DRC inaishutumu jirani yake Rwanda kwa kuwaunga mkono waasi wa M23, jambo ambalo Kigali imekuwa ikikanusha.

Post a Comment

0 Comments