Rwanda imemtoza mshatakiwa faini ya dola 900 kwa kosa la kifo cha mwandishi wa habari

 



Mahakama nchini Rwanda imemtoza faini ya $900 (£746) mwanamume mmoja baada ya kukiri kosa la kuua bila kukusudia kutokana na kifo cha mwandishi wa habari aliyekuwa akiikosoa serikali.


John Williams Ntwali aliuawa mwezi uliopita baada ya gari la mwendo kasi kugonga pikipikiki ya abiria aliyokuwa amepanda.


Mamlaka ilisema ilikuwa ajali ya barabarani. Mashirika ya kutetea haki za binadamu yaliitisha uchunguzi huru, yakielezea kifo chake kuwa cha kutiliwa shaka.


Human Rights Watch ilisema Bw Ntwali amekuwa akitishwa mara kwa mara na kushambuliwa katika vyombo vya habari vinavyounga mkono serikali kutokana na ripoti yake ya uchunguzi.


Kesi hiyo haikuwa wazi kwa umma lakini baadhi ya waandishi wa habari walialikwa kushuhudia kusomwa kwa hukumu hiyo.

Post a Comment

0 Comments