Tetemeko kubwa la ardhi lakumba Uturuki, kusini-mashariki karibu na mpaka wa Syria

 


Tetemeko kubwa la ardhi limekumba Gaziantep kusini-mashariki mwa Uturuki, karibu na mpaka na Syria na kuua takriban watu watano.


Utafiti wa Jiolojia wa Marekani ulisema tetemeko hilo la kipimo cha 7.8 lilitokea saa 04:17 saa za ndani (01:17 GMT) katika kina cha kilomita 17.9 (maili 11) karibu na mji wa Gaziantep.


Tetemeko hilo lilisikika katika mji mkuu Ankara na miji mingine ya Uturuki, na pia katika eneo zima.


Idadi ya majengo yameporomoka, na baadhi ya watu huenda wamenaswa.


Mwandishi wa BBC Kituruki aliyeko Diyarbakir anaripoti kuwa jengo moja la maduka mjini humo liliporomoka. Rushdi Abualouf, mtayarishaji wa BBC katika Ukanda wa Gaza, alisema kulikuwa na takriban sekunde 45 za kutikisika katika nyumba aliyokuwa akiishi.


Wataalamu wa tetemeko la ardhi wa Uturuki walikadiria nguvu ya tetemeko hilo kuwa ya kipimo cha 7.4. Walisema kuwa tetemeko la pili lilipiga eneo hilo dakika chache baadaye.


Uturuki iko katika mojawapo ya ukanda wa maeneo yenye tetemeko la ardhi duniani. Mnamo 1999, zaidi ya watu 17,000 waliuawa baada ya tetemeko kubwa lililotikisa kaskazini-magharibi mwa nchi.

Post a Comment

0 Comments