Ulaya yaweka marufuku kwa mafuta ya dizeli ya Russia

 


Ulaya Jumapili imeweka marufuku kwa mafuta ya dizeli ya Russia na bidhaa nyingine za mafuta yaliyosafishwa, ikipunguza utegemezi wa nishati ya Moscow na kutafuta kupunguza zaidi mapato ya mafuta ghafi ya Kremlin kama adhabu kwa kuivamia Ukraine.


Marufuku hiyo inajiri sambamba na bei ya kikomo iliyokubaliwa na kundi la nchi 7 washirika wa Ulaya.


Lengo ni kuruhusu mafuta ya dizeli yaendelee kusafirishwa kwa wingi katika nchi kama China na India na kuepuka kupanda ghafla kwa bei ambako kutaathiri wanunuzi duniani kote, huku marufuku hiyo ikipunguza mapato yanayofadhili bajeti na vita vya Moscow.


Mafuta ya dizeli ni muhimu kwa uchumi wa Russia kwa sababu yanatumiwa na gari, malori yanayobeba bidhaa, vifaa vya kilimo na mashine za viwanda.

Post a Comment

0 Comments