https://monetag.com/?ref_id=TTIb Mahakama ya juu Nigeria yatupilia mbali kesi ya kutaka kumuondoa rais mteule Bola Tinubu | Muungwana BLOG

Mahakama ya juu Nigeria yatupilia mbali kesi ya kutaka kumuondoa rais mteule Bola Tinubu

 


Mahakama ya Juu nchini Nigeria imetupilia mbali kesi ya kutaka kumuondoa rais mteule Bola Tinubu na mgombea mwenza wake Kashim Shettima kama wagombea urais na makamu wa rais wa chama tawala cha All Progressives Congress (APC) katika uchaguzi wa rais wa Februari 2023.


Kesi hiyo iliyowasilishwa Julai mwaka jana na chama cha upinzani cha Peoples Democratic Party ilidai kuwa uteuzi wa Bw. Shettima kama mgombea mwenza wa Tinubu ulikuwa unakiuka katiba ya Nigeria.


Hata hivyo, jopo la wanachama watano wa mahakama ya juu zaidi mnamo Ijumaa liliamua kwamba kesi hiyo haina mashiko.


Majaji walisema kuwa Peoples Democratic Party haikuwa na uwezo wa kuanzisha kesi hiyo kwa vile sio mwanachama wa APC.


Kulikuwa na woga na wasiwasi mbele ya hukumu ya kihistoria ya Mahakama ya Juu Chama cha upinzani kilikuwa kimesema kuwa uteuzi wa Shettima kugombea nafasi ya makamu wa rais na kiti cha useneta wa Borno - wakati huo huo - ulikiuka sheria.


Lakini Jaji Adamu Jauro ambaye alitoa uamuzi mkuu, alibainisha kuwa PDP ilikuwa inaingilia masuala ya ndani ya chama kingine na akapiga faini ya N2 milioni (kama dola 4,300) juu yake.


Uamuzi wa Mahakama ya Juu sasa umeliweka suala hilo mahali pazuri na inaonekana kutoa muhuri wa mahakama wa kuidhinisha kuapishwa kwa rais mteule Bola Ahmed Tinubu na Makamu wa Rais mteule Kashim Shettima.


Wanatarajiwa kuapishwa Jumatatu Mei 29 wakati rais Muhammadu Buhari atakapoondoka madarakani baada ya kumaliza muhula wa nne wa nne.

Post a Comment

0 Comments