Mswada wa hijab wa Iran: Wanawake wanakabiliwa na kifungo cha miaka 10 jela kwa mavazi 'yasiofaa'

 


Bunge la Iran limepitisha mswada wenye utata ambao utaongeza vifungo vya jela na faini kwa wanawake na wasichana wanaokiuka kanuni zake kali za mavazi


Wale waliovaa "isivyofaa" wanakabiliwa na kifungo cha hadi miaka 10 chini ya mswada huo, ambao "kesi" ya miaka mitatu ilikubaliwa.


Bado inahitaji kuidhinishwa na Baraza la Walinzi ili kuwa sheria.


Hatua hiyo imekuja mwaka mmoja baada ya kuzuka maandamano ya kupinga kifo cha Mahsa Amini, ambaye alishikiliwa na polisi wa maadili kwa madai ya kuvaa hijabu isiyofaa.


Wanawake walichoma vitambaa vyao au kuvipeperusha hewani kwenye maandamano ya nchi nzima kupinga utawala wa nchi hiyo ambapo mamia ya watu waliripotiwa kuuawa katika msako mkali wa vikosi vya usalama.


Idadi inayoongezeka ya wanawake na wasichana wameacha kufunika nywele zao hadharani kabisa huku machafuko yakipungua, licha ya polisi wa maadili kurejea mitaani na kuwekwa kwa kamera za uchunguzi.


Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items