Venezuela yawatuma wanajeshi 11,000 kuchukua udhibiti wa gereza

 


Venezuela imetuma wanajeshi 11,000 kurejesha udhibiti wa moja ya magereza yake makubwa ambayo yalikuwa yamevamiwa na genge lenye nguvu la uhalifu.


Gereza la Tocoron, kaskazini mwa nchi, lilikuwa chini ya udhibiti wa genge kubwa la Tren de Aragua kwa miaka mingi.


Wanachama waliweza kutembea kwa uhuru katika gereza hilo, ambalo lilikuwa na vifaa kama hoteli ikiwa ni pamoja na bwawa na kuogolea , klabu ya usiku na bustani ndogo ya wanyama, vyombo vya habari vya ndani viliripoti.


Maafisa walisema wafungwa hao 6,000 watahamishiwa katika magereza mengine.


Wakazi wengi huru walikuwa wakiishi ndani ya gereza pamoja na wafungwa waliohukumiwa.Baada ya mamlaka kutangaza kwamba wafungwa wangehamishwa, baadhi ya watu walilia nje, wasijue ni wapi jamaa zao walio ndani ya gereza wangeenda.


"Nasubiri kusikia wanampeleka wapi mume wangu...nilikuwa nikiishi mle ndani, lakini walitufukuza," Gladys Hernandez aliambia shirika la habari la AFP.


Iliripoti kuwa waandishi wa habari waliona walinzi wakiwa wamebeba pikipiki, televisheni na microwave kutoka jela.


Katika taarifa iliyotumwa kwa X, iliyokuwa Twitter, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Venezuela iliwapongeza maafisa kwa kurejesha jela hiyo na kubomoa "kituo cha njama na uhalifu".

Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items