Vita vya Ukraine:Poland kusitisha kusambaza silaha kwa Ukraine


Mmoja wa washirika wakuu wa Ukraine, Poland, ametangaza kuwa haitasambaza tena silaha kwa nchi hiyo huku mzozo wa kidiplomasia kuhusu nafaka ukiongezeka.


Waziri mkuu wa taifa hilo alisema badala yake itajikita katika kujizatiti kwa silaha za kisasa zaidi.


Hatua hiyo inajiri huku mvutano kati ya mataifa hayo mawili ukiongezeka.


Siku ya Jumanne, Poland ilimwita balozi wa Ukraine kuhusu maoni yaliyotolewa na Rais Volodymyr Zelensky katika Umoja wa Mataifa.


Alisema baadhi ya mataifa yamejifanya kuwa na mshikamano na Ukraine, ambayo Warsaw ilishutumu kuwa "isiyo na haki kuhusu Poland, ambayo imeunga mkono Ukraine tangu siku za kwanza za vita".


Waziri Mkuu wa Poland, Mateusz Morawiecki, alitangaza uamuzi wa kutoipatia Ukraine tena silaha katika hotuba ya televisheni siku ya Jumatano baada ya siku ya mvutano unaoongezeka kwa kasi kati ya nchi hizo mbili kuhusu uagizaji wa nafaka kutoka nje.


Mzozo wa nafaka ulianza baada ya uvamizi kamili wa Urusi dhidi ya Ukraine kufunga njia kuu za meli za Bahari Nyeusi isipokuwa moja na kuilazimu Ukraine kutafuta njia mbadala za kusafiri nafaka yake kupitia nchi kavu .


Hilo nalo lilisababisha kiasi kikubwa cha nafaka kuishia Ulaya ya kati.


Kwa hiyo, Umoja wa Ulaya ulipiga marufuku kwa muda uagizaji wa nafaka katika nchi tano; Bulgaria, Hungaria, Poland, Romania na Slovakia kulinda wakulima wa ndani, ambao waliogopa nafaka ya Kiukreni ilikuwa ikipunguza bei ndani ya nchi.

Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items