Ghadhabu ya wenyeji baada ya miili minne kupatikana katika shamba moja nchini Kenya

 


Miili minne iligunduliwa siku ya Jumapili kwenye shamba lililoripotiwa kumilikiwa na jeshi la Kenya, jambo lililozua ghadhabu kutoka kwa wenyeji.


Vijana hao wanne wanadaiwa kuvamia shamba karibu na kambi ya Jeshi la Ulinzi la Kenya katika kaunti ya Uasin Gishu, eneo la Bonde la Ufa, kukusanya mahindi yaliyokuwa yamebakia kutokana na mavuno ya hivi majuzi walipodaiwa kukamatwa na kupigwa hadi kufa na walinzi wa shamba hilo Jumamosi usiku.


Wenyeji walisema kuwa baadhi ya miili hiyo ilikuwa na majeraha ya risasi.


Wanaume wengine wanne ambao pia walikuwa wamevamia shamba hilo wanaendelea kupata matibabu kutokana na majeraha yakiwemo majeraha ya risasi na michubuko katika hospitali ya eneo hilo.


Wenyeji wameonyesha hasira wakisema kuwa walinzi hao walipaswa kuwakamata vijana hao badala ya kuwaua .


“Walikuwa vijana maskini waliokuwa wakihangaika kutafuta riziki.Kukusanya mabaki ya mahindi ilikuwa ishara kwamba walikuwa maskini na walihitaji kusaidiwa lakini wasiuawe,” mwenyeji mmoja aliambia gazeti la kibinafsi la Standard.

Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items