Wanafunzi watatu wa Kipalestina wapigwa risasi karibu na chuo kikuu cha Marekani


 Familia za wanafunzi watatu wa Kipalestina waliopigwa risasi huko Vermont siku ya Jumamosi zimewataka polisi kuchunguza shambulio hilo kama uhalifu wa chuki.


Hisham Awartani, Tahseen Ahmed na Kinnan Abdalhamid walikabiliwa na kupigwa risasi na mtu karibu na Chuo Kikuu cha Vermont Campus, Polisi wa Burlington walisema.


Maafisa wanachunguza sababu inayowezekana ya shambulio hilo lakini walisema walikuwa wamevalia keffiyeh - skafu ya kitamaduni - na wakizungumza Kiarabu waliposhambuliwa.


Polisi wanamsaka mshukiwa.


Mkuu wa polisi wa Burlington Jon Mura alisema waathiriwa wawili wako katika hali nzuri ;wa tatu amepata majeraha mabaya zaidi.


Bw Abdalhamid, alitajwa na Chuo cha Haverford kama mmoja wa wanafunzi wake.Wengine wawili wametajwa kuwa mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Brown Bw Awartani na Bw Ahmed, anayesoma Chuo cha Trinity huko Connecticut.


Rich Price, mjomba wa mmoja wa waathiriwa, alisema wanaume hao watatu - wote wenye umri wa miaka 20 - walikuwa wakihudhuria karamu ya kuzaliwa kwa mtoto wa miaka minane.

Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items