Israel kuruhusu lori mbili za mafuta kuingia Gaza kwa siku


 Israel inasema itaruhusu lori mbili za mafuta kwa siku kuingia Ukanda wa Gaza, baada ya kushinikizwa na Marekani kufanya hivyo.


Afisa wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani anasema takriban lita 140,000 za mafuta zitaruhusiwa kuingia Gaza kila baada ya siku mbili.


Mengi ya mafuta hayo yatatumiwa na lori zinazopeleka misaada, kusaidia yale ya Umoja wa Mataifa kutoa huduma za maji na usafi wa mazingira, afisa huyo alisema.


Zilizosalia ni za simu na huduma za mtandao, ambazo zilikuwa zimekatika kutokana na ukosefu wa mafuta.


Siku ya Ijumaa, kampuni inayotoa mawasiliano ya Gaza ilisema kuwa huduma zake zilikuwa zikirejea baada ya kupokea mafuta kupitia Unrwa, shirika la Umoja wa Mataifa la wakimbizi wa Kipalestina.


Afisa huyo wa Marekani alisema Washington ilitoa shinikizo kubwa kwa Israel kufikia makubaliano haya ya mafuta.


Mpango huo ulikubaliwa kimsingi wiki zilizopita, afisa huyo aliongeza, lakini uliahirishwa na Israeli kwa sababu mbili.


Maafisa wa Israel waliiambia Marekani kwamba mafuta yalikuwa hayajaisha kusini mwa Gaza, na pia walitaka kusubiri na kuona kama wanaweza kujadiliana kwanza kuhusu mpango wa mateka wao wanaozuiliwa Gaza.

Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items