Katika ujumbe wa X ( zamani ikiitwa Twitter), jeshi la Israel limesema lilishambulia maeneo kadhaa katika ardhi ya Lebanon Jumatano.
Limesema miongoni mwa maeneo hayo ni pamoja na ghala la silaha, miundombinu ya kijeshi, vituo vya uchunguzi na maeneo ambayo wanamgambo wa Hezbollah walirusha makombora katika ardhi ya Israel.

