Mshauri wa wafanyabiashara TCCIA Manyara hatiani kwa kughushi.


Na John Walter -Babati

Mahakama ya Hakimu Mkazi Manyara imemhukumu Bw. RAMADHANI RASHID MSANGI ambaye ni Mshauri wa Wafanyabiashara mwajiriwa wa Chama cha wenye viwanda na kilimo Mkoa wa Manyara (Bussines consultant -TCCIA Manyara).

Mshtakiwa ameamuriwa kulipa kiasi cha shilingi 900,000/= au kwenda jela miaka mitatu. kwa kosa la kughushi  nyaraka  za malipo .

Hukumu hiyo dhidi ya  Ramadhani Rashid Msangi katika shauri la uhujumu uchumi Na. 05/2023, imetolewa chini ya Mhe. Martin Massao Hakimu Mkazi wa Mahakama  ya Manyara Machi 22, 2024.

Mshtakiwa alighushi nyaraka mbali mbali katika marejesho yake  kuonesha kuwa alihudhuria  na kuendesha mafunzo ya wajasiriamali yaliyofanyika wilayani Hana'ng kwa kipindi cha mwezi februari  na juni mwaka 2018 na kwamba alitumia kiasi cha shilingi 6,695,000/=   Kugharamia posho ya chakula , ukumbi na nauli kwa waliodaiwa kushiriki mafunzo hayo huku akijua taarifa hizo hazikuwa sahihi.

Mshtakiwa  amelipa  faini na kuachiwa huru na mahakama.

Post a Comment

0 Comments