RPC Manyara azindua kikundi cha ulinzi Maisaka B.



Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP), George Katabazi na timu yake, Machi 12, 2024,  amefanya ziara ya kutembelea na kukagua utendaji kazi wa vikundi vya ulinzi mtaa wa Maisaka Wilaya ya Babati Mkoani hapa 

Ambapo, amekabidhi hati ya cheti cha Pongezi kwa viongozi wa Kikundi cha Ulinzi Mtaa wa Maisaka 'B' Halmashauri ya Mji Babati, Mkoani Manyara kwa kuonesha ushirikiano na kufanya kazi kwa uaminifu na weledi kwa kushirikiana na  Jeshi la Polisi huku wakiishi kwa vitendo dhana na falsafa ya Polisi Jamii na Ulinzi Shirikishi mtaani

Akizungumza wakati akikabidhi cheti, SACP Katabazi, amewataka vikundi vya ulinzi kufanya kazi kwa kuzingatia Sheria bila ya kumuonea wala kumpendelea  mtu ili kuepuka malalamiko katika jamii

Amesema Jeshi la Polisi linahubiri dhana na falsafa ya Polisi jamii na ulinzi shirikishi Kila Leo ili kuimarisha vikundi vya ulinzi kuanzia ngazi ya kitongoji, Kijij, mtaa na kata.



Katika ziara yake Katabazi amefanya harambee ya kuchangia fedha kwa ajili ya mahitaji muhimu ya kikundi hicho ikiwemo filimbi, tochi na Makoti ambapo amewaomba na wadau wengine kujitokeza kusaidia vikundi vya kulinzi

Sambamba naye, mmoja wa Viongozi  wa Kikundi hicho amelipongeza Jeshi la Polisi kwa kutambua na kuthamini mchago wao na kutoa ahadi kuuendeleza na  kuwaelimisha vijana wengine kujiunga katika vikundi vya ulinzi ili kushirikiana na Polisi katika kutokomeza uhalifu katika jamii

" kwa niaba ya Kikundi nashukuru Jeshi la Polisi kutupa cheti cha Pongezi, tutajituma zaidi ili tupatiwe zawadi kubwa zaidi" amesema kiongozi Kikundi Maisaka 'B'


Naye Mkuu wa Kamisheni ya Polisi Jamii Manyara Kamishna Msaidizi (ACP) Kija Mkoyi, amewataka vijana hususani bodaboda kuunda vikundi vya ulinzi katika maeneo yao ili kuimarisha ulinzi na usalma wao na Mali zao

Jeshi la Polisi Mkoa wa Manyara limekuwa likihubiri dhana ya Polisi Jamii na Falsafa ya Ulinzi Shirikishi pamoja na  kutoa sifa na zawadi kwa kikundi kilichofanya vizuri ili kuleta  hamasa katika kuimarisha ulinzi na usalama wa raia na Mali jamii

Post a Comment

0 Comments