Na John Walter -Babati
Kuelekea kilele cha miaka 60 ya Muungano viongozi wa dini mbalimbali mkoani Manyara Leo april 26,2024 wameoliombea Taifa, Rais Samia Suluhu na serikali yake ili Tanzania iendelee kuwa na amani, upendo na mshikamano.
Shughuli hiyo iliyofanyika katika uwanja wa Tanzanite Kwaraa mjini Babati ilihudhuriwa na watumishi wa umma na wananchi wamejitokeza wakimuomba Mungu aendelee kuudumisha Muungano huo.
Aidha Viongozi hao wa Dini wameiomba Serikali kusikiliza kero mbalimbali zinazowakabili wananchi na kuzifanyia kazi ikiwa ni pamoja na kero za Maji Migogoro ya ardhi, changamoto ambazo zimekuwa sugu katika baadhi ya Maeneo mkoani hapa.
Katika maombi hayo Katibu Tawala wa mkoa wa Manyara Mariam Muhaji ametumia nafasi hiyo kutoa wito kwa viongozi hao wa dini kuendelea kukemea vitendo vya ukatili wa kijinsia ikiwemo ubakaji ambavyo vimekithiri mkoani humo pamoja na wananchi kuwa na hofu ya Mungu.
0 Comments