LATRA watangaza nauli za SGR Dar hadi Dodoma


Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (Latra), imetangaza rasmi nauli za abiria wa usafiri wa reli ya kisasa (SGR) kutoka Dar es Salaam hadi MakutuporaDodoma kuwa ni Sh 31,000 kwa watu wazima na watoto wa kuanzia umri wa miaka 4 hadi 12 wakilipa nusu gharama.

Aidha taarifa hiyo imeanisha kiwango cha nauli kwa usafiri huo ni pungufu kidogo kulinganisha na kinachotozwa na usafiri wa mabasi yanayotoka Dar es Salaam kwenda Dodoma, kwani mengi yanatoza Sh29,000 hadi Sh35,000 kulingana na aina ya daraja.





Post a Comment

0 Comments