Na John Walter-Hanang'
Mwenge wa Uhuru umeingia rasmi katika Wilaya ya Hanang leo Julai 18, 2025, ukitokea Wilaya ya Mbulu, ukiendelea na mbio zake za kitaifa kwa mwaka huu.
Katika mapokezi rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Hanang, Mheshimiwa Almish Hazal, alieleza kuwa mwenge huo utatembelea, utakagua, kufungua na kuweka mawe ya msingi kwenye jumla ya miradi nane yenye thamani ya shilingi bilioni 9.6.
0 Comments