F ‎Mwenge wa Uhuru waridhia miradi ya Bilioni 6.1 ‎Simanjiro. | Muungwana BLOG

‎Mwenge wa Uhuru waridhia miradi ya Bilioni 6.1 ‎Simanjiro.



Na John Walter -Simanjiro

‎ Mwenge wa Uhuru ukiwa wilayani Simanjiro umekimbizwa umbali wa kilomita 159 na kuzindua, kukagua na kuweka mawe ya msingi kwenye miradi  saba yenye thamani ya shilingi bilioni 6.1.

‎Miradi yote hiyo imepata kuridhiwa na kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2025, Ismail Ussi Fakii Lulandala.

‎Mkuu wa wilaya ya Simanjiro, akitoa taarifa kwa kiongozi huyo, amesema maelekezo yaliyotolewa yatafanyiwa kazi na kutekelezwa kwa wakati ili kuhakikisha manufaa ya miradi hiyo yanafika kwa wananchi.

‎Kuhusu afya, imeelezwa kuwa jumla ya watu 113 walipimwa virusi vya UKIMWI wakiwemo wanawake 24 na wanaume 89, ambapo mwanaume mmoja alikutwa na maambukizi.

‎Vilevile, watu 37 walipimwa malaria na hakuna aliyeonekana na ugonjwa huo, huku watu 14 wakijitolea kuchangia damu kwa hiari.

‎Mwenge wa Uhuru unaendelea na mbio zake mkoani Manyara ukiwa na kaulimbiu "tujitokeze kushiriki  uchaguzi mkuu kwa amani na utulivu"

Post a Comment

0 Comments