Mbinu tatu (3) za kumtongoza msichana ili akubali mapema

Miongoni mwa maswali ambayo huwachanganya wavulana wengi ni pamoja ni kwa jinsi gani anaweza kumtongoza msichana na hatimaye akakubali. Wengi wao wanakuwa hawana ile nguvu ya kujiamini  ya kumtongoza msichana huyo macho kwa macho, wengi wao utawasikia ooh samahani naomba namba yako.

Sasa ili kuwaponya madomo zenge walio wengi hii ndiyo tiba ya kumtongoza mrembo yeyote hatimaye akakukubali.

1. Usimfanye ajue unampenda kwa dhati.

Wanaume wengi huwa wanafanyaga kosa hili kubwa . Wanawaambia wanawake wanawapenda au wanahisia za kimapenzi kwao . Ni kweli unampenda , anajua hivyo tayari . Au hajui ? Unampigia simu kila saa , mnataniani kimapenzi na anaona uhusiano wenu kabisa .

Kwahiyo japokua anahisi unampenda , usije kuonyesha hivyo kwani anahitaji kusikia kutoka kwako ili ajihakikishia hisia zake . Chukulia poa na usifunguke kuhusu hisia zako kwake , kitendawili alichonacho ndicho kitamfanya azidi kukunata na kutaka kujua mwisho wa mambo .

2. Ishi Maisha mawili

Unapoongea nae usiku , mwaga sera zako na funguka kuhusu mambo ya mapenzi sema mkikutana ana kwa ana mchana usiongelee mambo ya mapenzi kabisa labda aanze yeye na hivyo kumaanisha ashaingia line na anapenda maongezi hayo .

Pia epuka kuongelea kuhusu mambo yenu ya kimapenzi mnapokua na marafiki wengine bali fanyeni hivyo mkiwa wawili . Kwa kufanya hivyo unamfanya aamini kuna uhusiano motomoto wa siri unapikika kati yenu

3. Kuwa karibu na mtu huyo.
Siku zote , kama unataka kumtokea msichana njia muhimu kabisa ni kuweza kumjua kwa undani .Usikurupuke kurupuke tu ukaanza kutongoza , msichana ataogopa au atakuona mtu rahisi kua nae na mwisho wa siku utaishia kumboa tu .

Ongea nae na upate kumjua vizuri . Mtumie message na usiwe na mzuka , mfanye awe kama rafiki kwanza . Usimtokee kwanza sema pia usisubiri sana maana ataanza kukuchukulia poa .

Ukitumia mbinu hizo tatu nina imani kubwa ni lazima msichana huyo utampata tu.

Endelea kutembelea Muungwana Blog kila wakati.