Shirika linalofuatilia masuala ya mateka wa Kipalestina
limetoa ripoti mpya inayosema kuwa, zaidi ya Wapalestina 6000 wanaendelea
kuteseka katika jela za kuogofya za utawala haramu wa Israel . Qadura Fares, mkuu wa
shirika hilo
amesema wakati wa kutoa ripoti hiyo kuwa, Wapalestina wanapata mateso makubwa
katika jela za Wazayuni na haki zao za kimsingi zinakiukwa.
Baadhi ya wafungwa hao ni watoto walio chini ya umri wa
miaka 15. Hii ni katika hali ambayo, utawala haramu wa Kizayuni siku chache
zilizopita ulipitisha sheria ya kuwaruhusu askari wake wa magereza kuwalisha
kwa nguvu wafungwa wa Kipalestina wanaogoma kula wakilalamikia mateso dhidi yao .
Jumuiya ya Nchi za Kiarabu pia imezungumzia sheria hiyo kandamizi
ya Israel
ikisema kuwa, sheria hiyo ni ya kibaguzi na yenye lengo la kuficha mateso ya
Wazayuni kwa wafungwa wa Palestina.
