Hafla Ya Uwekaji Wa Jiwe La Msingi La Ujenzi Wa Ukuta Wa Ukingo Wa Bahari Hapo Mizingani Forodhani Mjini Zanzibar

  Makamu wa Pili a Rais wa Zanzibar Balozi Seif akiweka jiwe la Msingi la Ujenzi wa Ukuta wa kuzuia maji ya Bahari hapo Mizingani Forodhani Mjini Zanzibar ikiwa ni shamra shamra za kusherehekea miaka 53 ya Mapinduzi ya Zanzibar. Wa kwanza kushoto ni Waziri wa Fedha na Mipango wa SMZ Dr. Khalid Salum Mohamed ambapo wa nyuma yake ni Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mh. Zubeir Ali Maulid.

 Mandhari nzuri ya kuvutia ya muonekano wa Ukuta wa kuzuia maji ya Bahari hapo Mizingani Forodhani Mjini Zanzibar  ambapo ujenzi wake umewekwa jiwe la Msingi  na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi.

  Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Utunzaji na Uhifadhi wa Mji Mkongwe wa Zanzibar Nd. Issa Sarboko Makaran akimpatia maelezo Balozi Seif jinsi ya wajenzi wa Ukuta wa Kuzuia Maji ya Bahari Mizingani wanavyozingatia  uhifadhi wa urithi wa Dunia uliomo ndani ya Mji Mkonhgwe.

  Balozi Seif akizungumza na Wananchi katika hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa Ukuta wa kuzuia maji ya Bahari hapo Mizingani Forodhani Mjini Zanzibar.

Kikundi cha Utamaduni cha Mkoa wa Mjini Mgharibi kikifanya vitu vyake wakati wa kutoa burdani kwenye hafla ya ya uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa Ukuta wa kuzuia maji ya Bahari hapo Mizingani Forodhani Mjini Zanzibar.
Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items