Uwanja wa ndege wa Madeira utapewa jina la Cristiano Ronaldo ili kumpa heshima mshindi huyo wa mataji Ligi ya Mabingwa Ulaya, La Liga, Ligi Kuu England na kusumbuana mno na Lionel Messi katika kuwania Ballon D'Or miaka michache iliyopita. Utambulisho rasmi kwa Uwanja huo kwa jina lka Ranaldo utafanyika Machi 29, siku ambayo Ureno itamenyana na Sweden mjini Funchal.
