Beki aliyemaliza mkataba wake Yanga, Haji Mwinyi amesema kuanguliwa kwa katika kikosi cha Taifa Stars, kumenyima posho pamoja na kujulikana kimataifa.
Mwinyi ni miongoni mwa wachezaji wa Zanzibar waliondolea katika kikosi cha Stars kilichoenda
Misri kujiandaa na mechi ya kusaka kufuzu kwa AFCON2019, dhidi ya Lesotho itakayocheza Juni 10, mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mwinyi alisema hasara za kuenguliwa Stars ni kukosa posho zinazotolewa kwa wachezaji wanaokuwa kambini na timu hiyo.
"Tumeondolewa kutokana na Zanzibar kuwa mwanachama wa CAF ni jambo zuri, kwani imefika wakati wa Wazanzibari, kujitangaza wenyewe hivyo viongozi wanatakiwa kuweka utaratibu mzuri wa kujua tutanufaika vipi," anasema
Mbali na posho, beki huyo anasema mchezaji anayechezea timu ya taifa, anakuwa anajulikana na mataifa mbalimbali,hivyo inakuwa rahisi kupata dili nje.
"Jambo la kujivunia baadaye kwamba nilifanya kitu katika taifa kama wanavyotolewa mfano kina Leodegar Tenga, wanaoonekana mfano kwenye taswira ya soka," anasema.
